MABINGWA WA KUDANGANYA WHATSAPP, DAWA IMESHAPATIKANA!

Kuanzia sasa ujumbe ambao tayari umepokelewa na kusomwa utakuwa unaonesha tiki mbili za blue upande wa kulia chini kwenye simu ya mtumaji, na uki bonyeza juu ya ujumbe huo itakuwa ikionesha muda ambao ujumbe huo ulisomwa. 
Whatsapp wamewapunguzia sababu ya kujitetea wale wote wenye tabia za kutojibu message kwa kisingizio kuwa hawakuziona hata kama zilionesha tiki mbili kuashiaria zimefika. Sasa Whats App imeongeza alama ya kuonesha kuwa ujumbe umesomwa na muda ambao umesomwa.
Kabla ya maboresho hayo kulikuwa na aina mbili tu za tiki, tiki moja ya kijivu ilikua ikionesha ujumbe umetumwa, tiki mbili za kijivu ziliashiria ujumbe umefika.
Upande wa messages za group, tiki mbili za blue zitakuwa zikionekana pindi tu watu wote kwenye group wakiusoma ujumbe.
Ili kuona mabadiliko hayo, mtumiaji wa Whatsapp anapaswa ku update app hiyo kwenye simu yake.

Comments

Popular posts from this blog

10 Celebs Who Killed Their Careers After Dissing Beyonce

65 Home Business Ideas You Can Do From Your Kitchen Table

Top 7 Must Watch Tv Shows about Money and Business