MUME WA FROLA MBASHA ATUHUMIWA KUMBAKA SHEMEJI YAKE
Dar
 es Salaam.Mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili,  anatuhumiwa 
kumbaka shemeji yake mdogo 17.Taarifa za tukio hilo ziliripotiwa juzi 
saa 12 jioni katika Kituo cha Polisi Tabata (Tabata Shule), zikimtuhumu 
mwanamume huyo kwamba alimbaka binti huyo mara tatu na kumsababishia 
maumivu makali.
Binti
 huyo alifika katika kituo hicho cha polisi akiwa na ndugu zake wawili 
ambao walilalamika kwamba kulikuwa na jitihada kubwa kutoka upande wa 
mtuhumiwa wa kuzima kesi hiyo.
Akizungumza
 na blog hili nje ya kituo hicho, binti huyo alisema shemejiye alimbaka 
mara ya kwanza, Ijumaa iliyopita na Jumapili alipombaka mara mbili ndani
 ya gari.
Alisema
 mara ya kwanza alikaa kimya baada ya mtuhumiwa kumtishia kwamba 
angemdhuru kama angetoa taarifa ya tukio hilo alilofanyiwa wakiwa 
sebuleni nyumbani kwako Tabata Kimanga, lakini aliamua kutoa taarifa kwa
 ndugu zake baada ya kubakwa mara ya pili.
Polisi
 katika kituo hicho walithibitisha kupokea taarifa za tukio hilo lakini 
walishindwa kwenda kumkamata mtuhumiwa kwa maelezo kwamba hawakuwa na 
askari wa kutosha na kuahidi kwamba angekamatwa jana. Hata hivyo, hadi 
jana mtuhumiwa huyo alikuwa hajakamatwa.
Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi kutwa nzima ya jana 
hakupatikana kuzungumzia tukio hilo na kila simu yake ilipopigwa (kati 
ya saa nane mchana na saa mbili usiku), ilipokewa na msaidizi wake 
akisema bosi wake ana kazi nyingine.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema hakuwa amepokea taarifa yoyote ya aina hiyo.
Mwimbaji anena
Alipoulizwa
 jana, mwimbaji huyo alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia kwa undani 
tuhuma zinazomkabili mumewe na kwamba alikuwa anajisikia vibaya kutokana
 na tukio hilo kuhusisha watu wake wa karibu.
“Of
 course (bila shaka), hili sio tukio zuri. Kwa sasa sina uwezo wa 
kuzungumza kwa sababu hili suala lipo Polisi. I am confused 
(nimechanganyikiwa), ukizingatia kwamba linasemekana kutokea wakati 
sikuwepo nyumbani, naomba tuzungumze baada ya akili kutulia,” alisema.
Kadhalika,
 jana saa 6:20 mchana, gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza na mtuhumiwa 
ambaye baada ya kupewa maelezo kuhusu tuhuma zinazomkabili alisema: 
“Samahani sana ujue sikusikii kabisa,” kisha alikata simu.
                                                                                          
SOURCE:SINTAH
Sijui ndo nyakati za mwisho, sijui ndo kupitiwa na shetan????
Mungu amuongoze na kumpa nguvu huyo mtoto. 
Comments
Post a Comment