Wakatoliki wakataa kuwatambua mashoga.
Makundi ya kikatoliki yanayopigania 
haki za wapenzi wa jinsia moja yameelezea ghadhabu yao kutokana na hatua
 ya maaskofu wa kanisa hilo ya kukataa mapendekezo ya kutangaza msimamo 
kuhusu mashoga, wasagaji pamoja na watu waliotalakiana na wanaoana.
Wakati
 wa kumalizika kwa mkutano wa maaskofu wa kanisa katoliki, Vatican 
ilishindwa kupata theluthi mbili ya kura za maskofu wa kuunga mkono 
maoni yao kuhusu masuala hayo.Kundi la kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja nchini Marekani la New Ways Ministry limesema kuwa hatua ya maskofu hao kuamua kujadili suala hilo ni matumaini ya siku za usoni.
Masuala hayo yanatarajiwa kuzungumziwa tena baada ya mwaka mmoja.
Comments
Post a Comment