MAREKANI: WAZIRI WA ULINZI CHUCK HAGEL AJIUZULU
Barack obama amekubali Jumatatu Novemba 24 ombi la kujiuzulu kwa waziri wake wa ulinzi, Chuk Hagel.
Waziri wa
 ulinzi wa Marekani Chuck Hagel, amewasilisha barua yake ya kujiuzulu 
Jumatatu Novemba kwenye Ikulu ya Washington. Kujiuzulu huko kumetangazwa
 na Chuck Hagel wakati wa mkutano na vyombo vya habari, mkutano ambao 
umehudhuriwa na barack Obama.
Kulingana na 
kauli ya Barack Obama, Chuk Hagel ndiye ametaka mwenyewe kutamatisha 
muhula wake kwenye wadhifa aliyokua akishikilia. Kati ya wawili hao 
hakuna aliyetoa maelezo zaidi kuhusu uamzi huo wa kujiuzulu. Lakini kwa 
mujibu wa vyombo vya habari vya Marekani, waziri wa ulinzi alikua 
alipewa shinikizo.
Gazeti la
 New York Times limebaini kwamba kujiuzulu kwa Chuk Hagel kunahusiana na
 hali ya kutoelewana iliyojitokeza katika vita vinavyoendeshwa na 
Marekani dhidi ya kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislam nchini Iraq na 
Syria.
Inasadikiwa
 kuwa Ikulu ya washington huenda ilikua ikitathmini mkakati wake dhidi 
ya wanajihadi na ilikua inahitaji mkakati huo uanze kutekelezwa na 
waziri mpya wa ulinzi. Chuck Hagel awali alikuwa na wajibu wa kusimamia 
uondoaji wa majeshi kutoka Iraq na Afghanistan, wala si kusimamia 
operesheni ya kijeshi.
Washirika
 wa karibu wa Barack Obama wamekanusha hoja ya kujiuzulu kutokana na 
kushinikizwa. " Hakuna tofauti ya maoni ambayo imesababisha Chuk hagel 
anachukua umazi huo wa kujiuzulu", maafisa wa Ikulu ya Washington 
wamesema. Maafisa hao wamebaini kwamba mazungumzo ya kujiuzulu kwa Chuk 
Hagel yalianza wiki mbili zilizopita.
Waziri wa
 Ulinzi ataendelea kushikilia wadhifa huo hadi atakapopatikana mrithi 
wake. Majina kadhaa tayari yameanza kutajwa, ikiwa ni pamoja na Michèle 
Fournoy, aliyekuwa naibu waziri wa ulinzi.
Comments
Post a Comment