RAIS OBAMA ASIFU UVAAJI WA FULANA YA I CAN'T BREATHE ALIYOVAA MCHEZAJI WA KIKAKPU LEBRON JAMES
Rais wa Marekani Mhe. Barack Obama amesifia uvaaji wa fulana wa 
mchezaji wa mpira wa kikapu Lebron James wakati alipokua akifanyiwa 
mahojiano na gazeti la the people magazine. Rais Barack Obama alipouliwa
 swali hilo nini mtizamo wake alisema nadhani ni jambo zuri kwa mchezaji
 huyo na wengine waliopaza sauti zao kuwakilisha mawazo yao kwa mambo 
yaliyotokea ya kuuwawa kwa Wamarekani weusi na polisi huko Ferguson 
jimbo la Missouri na Brooklyn New York na baadae mahakama kuwaachia huru
 polisi hao waliofanya mauaji hayo kwamba walikua wakitekeleza wajibu 
wao wa kazi.
I can;t Breathe ni maneno ya mwisho aliyeongea Eric Garner kabla ya 
kukata roho baada ya kukabwa koo na polisi wakati walipokua wamekwenda 
kumtia mbaroni.
Comments
Post a Comment